Wednesday, August 3, 2016

Maudhui ya riwaya kwa kuzingatia mkondo wa kimapinduzi


MKONDO WA KIMAPINDUZI
Kwa muujibu wa Madumulla (2009:69) anasema ni mkondo ambao hujadili matatizo ya kisiasa ikiwa na mwelekeo fulani wa kuleta mabadiliko ya kisiasa na jamii. Ni mkondo unaozungumzia mabadiliko ya kisiasa katika jamii, wnanchi wakitaka kupigania haki zao na kuleta mabadiliko katika jamii.

Sababu zakutokea kwa mkondo huu ni mabadiliko ya Kisiasa, watu kutaka kudai haki zao na ulitokea katika miaka ya sabini.

Riwaya zilizoandikwa wakati huo ziliongelea mnyonge kuchukua silaha kupambana na mwenye nguvu ili kupigania haki zao, mkondo huu ulikuwa umekusudia kuleta usawa na haki katika jamii. Mfano: wa riwaya katika mkondo huu ni kuli iliyoandikwa na Shafi Adam Shafi, Nyota ya Rehema, Kasri ya Mwinyifuad, Giza katika Nuru, Utengano iliyoandikwa na A.J. Saffari, Vuta n'kuvute iliyoandikwa na Mohammed. S. Khatibu.

MAUDHUI YA RIWAYA KATIKA MKONDO WA KIMAPINDUZI.
Binadamu hutazamwa kama zoon politikon, yaani mnyama wa kisiasa, Mnyama mwenye uwezo wa kupatana.
Baadhi ya riwaya kuweka mkazo katika itikadi kama msingi au dira ya kuielekeza jamii.
Husisitiza umuhimu wakuwa na msimamo na mwelekeo.
Kwa mfano: Katika kitabu cha vuta n'kuvute mwandishi ametumia muhusika Denge kuonesha msimamo kwa kutetea haki ya watu weusi dhidi ya watu weupe au wakoloni. Vile vile katika kitabu cha Dunia mti mkavu – kilichoandikwa na Said Mohamed, amewatumia wahusika Mashaka na Bakari kuonesha jinsi walivyopigania haki za uma. mfano: kuiba chakula kwaajili ya uma.
Umuhimu wa uma kuleta mapinduzi.
Kwa mfano katika kitabu cha vuta nikuvute kilichoandikwa na Shafi Adam Shafi; ametumia mhusika Denge na wahusika wengine kama Chande, Mambo na Yasimine walivyoweza kuandaa vipeperushi mbalimbali kwaajili ya kuelimisha jamii, ili kuiondoa madarakani serikali ya kikoloni kwa ajili ya ukombozi wa mtu mweusi.
Usawa wa binadamu.
Hapa waandishi mbalimbali wanajaribu kuonesha jinsi binadamu wanavyotakiwa kuhusiana na kushirikiana katika jamii bila kujali tofauti zao.
Mfano; Katika kitabu cha takadini; mwandishi amemtumia mhusika Sekai alivyojaribu kupigania haki ya walemavu wa ngozi, hasa kumtorosha mwanae.
Mapinduzi kupatikana hata kwa njia ya mapambano.
Kwa mfano: Katika kitabu cha vuta nikuvute kilichoandikwa na Shafi Adam Shafi. Mwandishi amemtumia mhusika Denge kuonesha jinsi ambavyo amejitoa mhanga kupamabana katika kuleta mapinduzi. Hii inadhihirika pale ambapo mhusika Denge apambana hadi kufungwa gerezani.

Demokrasia ya uma. Riwaya nyingi za kimapinduzi zinasisitiza sana uwepo wa demokrasia ya kauli kwa jamii husika. Hii ina kuwa usawa na haki uzingatiwe kwa wanajamii bila kujali matabaka yao.
Kwa mfano katika kitabu cha adili na nduguze, kilichoandikwa na Shabani Robert. aliyewatumia wahusika manyani kuonyesha jinsi walivyokuwa wakihangaika kudai haki zao, wao kama tabaka la chini na majini wakiwa tabaka la juu. Hivyo manyani walikuwa wakidai haki, na usawa toka kwa majini (wakoloni).

muundo wa mbinu katika mkondo wa kimapinduzi
Wahusika ambao wanatoa mwanga kuhusu mwelekeo na wenye msimamo wa kuelewa hali ya matatizo ya kijamii, kihistoria, kisiasa na kiuchumi.
Kwa mfano: katika kitabu cha takadini kilichoandikwa na Ben Hanson mwandishi amemtumia muhusika Sekai amefanikiwa kuonesha mwelekeo kuwa mulemavu wa ngozi sio kwamba atazaa walemavu wa ngozi.

Hujaribu kuepuka mawazo mufilisi
Mawazo hayo ni kama vile mapenzi, ujamabzi na mijadara kuhusu Mungu. Kwa mfano; katika kitabu cha Vuta nikuvute, mtunzi amemtumia muhusika Denge kuonyesha kuepuka mawazo mufilisi. Denge alikataa kujihusisha kimapenzi na Yasmini vile vile mwandishi katika kitabu hiki hajazungumzia suala la ujambazi na mijadala kuhusu Mungu.
Lugha huwa rahisi inayoweka matatizo bayana bila kificho
Kwa mfano; katika kitabu cha Watoto wa Mama Ntilie, kilichoandikwa na Emmanuel Mbogo ametumia lugha rahisi inayoweka wazi matatizo ya kijamii kama vile umasikini, uonevu na unyanyasaji.
Suluhisho kwa kawaida ni la kijamaa au kisoshalisti katika riwaya za kimapinduzi.

MAREJELEO:
Madumulla, J. S (2009) Riwaya ya Kiswahili, Nadharia, Historia na Misingi ya uchambuzi. Dar es Salaam Tanzania: Mture Educational publishers Ltd.
Kitabu cha vuta n'kuvute
Kitabu cha takadini
Kitabu cha Watotot wa mama ntilie
Kitabu cha dunia mti mkavu
Adili na nduguze

No comments:

Post a Comment

hakiki na tuma maoni au mapendekezo kuhusu makala hii ya andiko langu la uchunguandiko langu

ANDIKO LA UCHUNGU (Kwa shemeji zangu na wanangu)           NYAMBUYA OGUCHU,                            S.L.P 777666,       ...