Tuesday, July 5, 2016

Ulinganishaji wa tanzu za fasihi simulizi ya kiswahili na ile ya kibantu.

Ulinganishaji wa fasihi simulizi ya kiswahili na ile ya kibantu 
                    
a)       Mifano ya methali katika lugha ya Kizinza
  1. Kizinza : Ente elikwilagula, kukamwa amata galikwela.
Kiswahili : Ng’ombe mweusi kukamuliwa maziwa meupe.
  1. Kizinza : Ibhale kumela, litene muzi.
Kiswahili : Jiwe kuota bila mzizi.
  1. Kizinza : Enzemu kuzala, etene mukwata.
Kiswahili : Mgomba kuzaa bila mume.
  1. Kizinza : Enkoko kwoncha, etene mabhele.
Kiswahili : Kuku kunyonysha bila matiti.
  1. Kizinza : Enzoka kulibata, etene magulu.
Kiswahili : nyoka kutembea bila miguu.


  1. Vitendawili. Mifano ya vitendawili katika lugha ya Kizinza
  1. Kizinza : Ntela enchitasimbuka…………. (ensimbazi).
Kiswahili : Napiga kisichostuka…………… (giza).
  1. Kizinza : Ndibata nechitandindila………… (omuhanda)
Kiswahili : Natembea na kisichinisubuli ………. (njia)
  1. Kizinza : Tinyihamo omo tindya…………….. (amahiga)
Kiswahili : Nitowapo moja huwa sili……….. (mafiga)
  1. Kizinza : Ahotulyaha omukama noha…………(omulilo)
Kiswahili : Tulipo hapa mfalme ni nani……….... (moto)
  1. Kizinza : Naho mwanawe elabha…………. (ihulu lyenzu)
Kiswahili : Lakini wewe mtoto huangalia………….. (tundu la nyumba)
(c) Nyimbo. Mfano wa wimbo wa harusi katika lugha ya Kizinza
OLUZINA LWOBWENGA
Yahuwee yahuwee yahuwee abhalonzi babayo,
Kuswelwa omuseza mubhi amuhanda omwibembeza,
Tibabhuza ogwo ni balo imbagambila nomukozi akola ahamuka,
Yahuwee yahuwee yahuwee abhalonzi babayo x2
WIMBO WA HARUSI
Jamaniee jamaniee jamaniee watafutaji huwa wapo,
Kuolewa na mwanaume mbaya njiani unamtanguliza,
Wakikuuliza huyo ni mmeo nawambia ni kijakazi hufanya kazi nyumbani,
Jamaniee jamaniee jamaniee watafutaji huwa wapo
Kamuoa mwanamke mbaya njiani unamtanguliza
Wakiuliza huyo ni mkeo nawambia ni kijakazi hufanya kazi za nyumbani.
Jamaniee jamaniee jamaniee watafuataji huwa wapo x2


  1. Hotuba. Mfano wa hotuba katika lugha ya kikinga
ILITATIZO LYA UVUHAVI PA KIJIJI
Valokholo vanakijiji nditegemela mgemila ilelo ndyemle mbele jinyo ukhocho vevela ilitatizolya uvuhav. Ilikhomela pa kijiji kyawe.
Valokholo vanakijiji, avahenga vakhecho tchovile khame nauzibili uvufa jou tchenga uvukuta kwani khememetuzuile ihtatizo lya uvukhevi pa kijiji kyawe jokhijaga.
Valokholo vanakijiji ifikhuizi tchapakheribu khuomie na matukio kha khudwatcha. Aghivionesa uvuhavi pa kijiji kyawe moja ya mambo hayo ni
Ukujagha khwa vana; valokholo vana kijiji, nditeghemela voni. Mpolike etaarifa ja ukhuijaghakwa vana mu mazingira kha khutatanisha. Umwana wa Mgogolo Chimbuzi akhojaghile akhepindi chya khutchunga, umwana wa mkokolo Ngolole akhaagile pa kisima pamoja kno mwana wa mkokolo Luhenda akhojagila ikhepindi hela kya. Kuhegala inyagala.
Khuvonekha khwa emisukule; valokholo vanakijiji, pa kijiji kyawe pavie na amatatizo gha kuonekha kwa avanu avsue khatale, thotsi avana view. Uvuvakhamila khosyole vakhambwene u bwana Luhelwa Uvakhasue e miaka khadatu igigendile, tena e wiki eji ghendile u mama Luchululu akhevonikha pa njia panda ja khuluta pa khesima akhielenga avanu.
Elitatizo lya khogona panzi; valokhelo vanakijiji avahenga khogona panzi valokhilo vanakhejiji avahenga vakhtcho vile ovibela panonu pavivi pivivi pikhomwelanga. Vanakhejiji tuvonekha natunogwa avanavawe vasome esyole basi avamo vame juvikhwendelea khuva va pelwapelwa ekhijiji kyawe jokhikhosa amaendeleo na khuzidiwa na ekhejiji kya Mavanga. Khwani avanu avoviletw khusomesa avana vawe vikhoneswa khonzi kha mibuya khehavi mumbale na lywangwa kipuera na muvivanza.
Vavokholo vanakhejiji, khama onende chifu pa khejiji kyame, khuanza za elelo avanu ovonivomba amamboghe uvuhavi valekhe mara moja khwani umunu ujikwibatwa ighaa uvughalaghela uvyo vywa ukuhani ji homya efrani ya eng’ombe moja ne eligunila lya uvyonga bakho pampja na ukhosema pa kijiji khyawe.
Mwalemi khwa, khumulisa, elisago iyane kwanye, khuvombela mbombo elimenyo iyototchonile elelo hapa mwalemi sana.
TATIZO LA UCHAWI KIJIJINI
Ndugu wanakijiji natumai hamjambo. Leo hii nimesimama mbele yenu kuzungumzia tatizo la uchawi linalokikabili kijiji chetu.
Ndugu wnakijiji, wahenga walisema usipoziba ufa utajenga ukuta kwani tusipodhibiti tatizo la uchawi kijiji chetu kitaangamia.
Ndugu wanakijiji, siku hizi karibuni kumekuwepo na matukio ya kutisha yanayodhihilisha uwepo wa uchawi kijijini kwetu. Matukio hayo ni kama yafuatayo:
Upotevu wa watoto; ndugu wnakijiji, nadhani wote mmesikia taarifa juu ya upotevu wa watoto watatu katika mazingira ya kutatanisha. Mtoto wa mzee Ngolole aliyepotelea kisimani pamoja na mtoto wa mzee Luhenda aliyepotelea wakati alipoenda kukusanya kuni.
Kuonekana kwa vizuka; ndugu wanakijiji, kijiji chetu kimekumbwa na tatizo la kuonekana kwa watu waliofariki zamani. Juzi wanetu walipokuwa wakitoka shuleni walimuona Bwana Luhelwa aliyefariki miaka mitatu iliyopita. Pia wiki iliyopita Mama Luchululu alionekana njia panda ya kwenda kisimani akiwaita watu.
Tatizo la kulazwa nje; ndugu wnakijiji, wahenga walisema mkataa pema pabaya namamwita. Wanakijiji, tunaonekana kwamba hatutaki watoto wetu wapate elimu hiyo wanetu wataendelea kuwa wajinga, hivyo kijiji chetu kitakosa maendeleo na kuzidiwa na kijiji cha Mavanga kwani wanaoletwa kutufundishia watoto wetu wanalazwa juu ya mibuyu, kando kando ya mto Kipewra na viwanjani.
Ndugu wanakijiji nikiwa kama chifu wa kijiji hiki, kuanzia sana wenye tabia hizo za uchawi waache mara moja kwani kwa atakayebainika kujihusiha na jinga huo atatozwa faini ya ng’ombe watano na unga gunia moja. Vilevile licha ya adhabu hiyo, mhusika lazima tumfukuze kijijini kwetu.
Akhsanteni kwa kunisikiliza ombi langu kwenu ni kuzingatia tuliyoyazungumza katika kikako hiki cha leo.
  1. Malumbano ya watani. Mfano wa malumbano ya watani katika lugha ya Kizinza
BHUCHIGULWA
Omwanya gwalofu nokunaga oluganda lwa bayungu na abheriri
Omuyungu : imulila chiha ogu achalikufa tali kunsekelela!
Omwiriri : nobuza chiha nimwe mwavita guku wenyu mbamutina kwobulozi echijiji chona niwe yamwita.
Omuyungu: ha! ha! ha! bhamwita nkahi oguahunile kwonka obhujanja bwenyu twabumannyile imubagambila abantu bhahunile ili mubone emichango leo tikuchangia omuntu alachanga ntutwala yona timukubona nesumani.
Omwiriri : twabamanyile imwita badugu bhetumuze kubakolesa omumashamba genyu, muketa tizibazomo twamsanga omwishamba lya kakawenyu nayembula amapo, tutukwikiliza mpaka mdugu wetu mumusubye muganya timlayanga kakawenyu ntumwihalo ebhicha.
Omuyungu : nemwe mwayebilwe nkokwo mulyaaba lozi, guku wawe akasangwa na sela ahabutuzi, nabakamgambila aite omwana womwe wobuzigezwa nikwo yamugambila ahunile abhantu bazile bhati yafa kumbe tiyafa. Mpa amenzi mulebhe talabha ataganywile.
Omwiriri: amenzi gachi naho nimwe mwatwitila mdugu wetu, lebha watukwilwe ameso kwobulozi.
Omnyunyu : talaba yafa itwenda ente, timlabha mutatulole ntumubaga nakumulya
Omwiriri : mubaletele embwa yabho bhehake
Omungungu : timwakulekile kutuha twakamubagile nokumulya omumeso genyu.
Omwiriri : mutulugile aha bhalozimwe mzende kulya akabwa kenyu
Omunyungu : twabakaza mutakusubhila kubagambila bhandugu bhenyu bahunile.
Twamala
MALUMBANO YA WATANI
Mfano wa kati wa msiba na mazishi yake kati ya ukoo wa bayungu na abheriri
Muyungu : mnalia nini? huyu hajafa mbona anacheka
Mwiriri : unauliza nini? Na wakati nyie ndo mmemuua, tena babu yako mchawi anayeogopwa kijiji kizima ndiye kamuua,
Muyungu: ha! ha! Ha! kauliwa wapi wakati kasinzia tu, na mbinu zenu tumeshazijua mmemwambia asinzie ili mpate mchango ya msiba, na leo hachangii mtuu, na akichangaa tunachukua michango yote, hampati hata sumuni.
Mwiriri : tabia zenu tuazijua mnaua ndugu zetu ili mkawafanyishe kazi huko mashambani kwenu. Mlimuua Tuzibazamo, tukamukuta shambani kwa bibi yako anavuna mahindi. Leo hatukubali mpaka mumfufua ndugu yetu, vinginevyo bibi yako tunamtua shingo.
Muyungu : na nyie mmesahau mlivyo wachawi, babu yako alikutwa anawanga kwa jirani na adhabu yake aliaambiwa amtoe kafara mwanae wa kwanza na ndiyo maana mmemwambia sinzie watu wajue amekufa kumbe hajafa. Lete maji nimunyweshe tuone kama hatokunywa.
Mwiriri : maji ya nini wakati nyie ndiyo mmetuulia ndugu yetu, ona macho yalivyo mekungu kwa sababu ya uchawi.
Muyungu: na kama amekufa tunataka ng’ombe, msipotoa tunamchinja na kumla.
Mwiriri : waleteeni mbwa wao wakafakamie
Muyungu : Msingetoa leo, mngeona tungemchinja na kumla mbele yenu
Mwiriri : tokeni wachawi wakubwa nendeni mkale hicho kimbwa chenu.
Muyungu : tumewakomesha ili msirudie kuwaambia ndugu zenu wasinzie.
Mwisho.
  1. Ngano za usuli. Mfano wa ngano za usuli katika lugha ya Kiha
IJOSI DYI MBUNI NI NGONA
Umcha migani: Ngane imigani…..!
Abhaganigwa : gana………!
Halabhaye, ingona ni mbuni bhali abhagenzi bhakundanye chane. Umwanya wose mbuni agiye kumgezi, yalamlasa muhaliwage ngona kulukuondo atalamwa amazi. Mbuni yalamthamini chane uwo mhali wage. Ingona yadya ibhikoko ni nzebha alikolelo ntiyashobhora kumdya mhali wage imbuni nu musi na umwe. Muwo mwanya imbuni yalabhanye ijosi ligufi hanyuma niyimisi.
Imisi yose ingona yategera ibhikoko bhije ukumwa amazi kuko yolonka ibhilibwa vyage na niyo hali ingeso yage. Aho lelo hali ingeso yage yukwinyegeza mumazi nu kwegela aho ibhikoko hibhili. Aho yarakidarukira igikoko kimwe nu kugifatisha amenyo yage nu kukibhulumlila mmazi kuja kukilila hiyo. Ahaze yalava mmugezi nu kugahrama kulusi ukota izubha hamwe nu mugezi.
Umusi umwe, ingona yalifise inzara chane, uwo musi yalategeye ibhikoko bhize nkimise yose lakini hali umusi mubhi iwage. Nta gikoko na kimwe chaziye ukumwa amazi. Inzara ikomoye yalaifashe ingona ntiyimenye chu gukora.Hiyari muwo mwanya yalamubhonye mgenzi wage mbuni hayaza, ntakundi nukumfata mhali wanje mbuni nukumdya aho ndo kila inzara yinfise, ingona yaliyumviye. Mbuni yalamwegeye umugenzi wage nu kumulamsa nkadyo vyalibhili, abhona umugenzi wage ngona nta shimwe afise nkadyo yali aho hanyuma. Mbuni avuga,
Mbuni : emugenzi wanje ufise iki?”
Ingona : Kuki? (kwi jwii dyi hefo nu dyu bhulushi)
Mbuni : hayambona ata shimwe ubhanye
Ingona : Idyenyo hayelindya chane
Mbuni : Idyenyo?
Ingona : ehe!, ndalindakutegeye uze ulilabhe umbwile nkadyo libhaye.
Mbuni : oooh!, hola chane, nuko lelo asama ndalilabhe.
Ingona : ehe, mhali wanje ni ndyenyo dya hanyuma nyene.
Imbuni yingije umutwe wage mumunwa wi ngona kulabha idyo dyenyo. Muwo mwanya nyene agizentyo, ingona yahweje ilumya umunwa wage nukwivuta ugusubhira mumazi. Imbuni nayo ilikoilagerageza kwivanamo. Yalagerageje ku nguvu zage zose gusubhila hanyuma. Aholelo imbuni hiyaliyivuta kusubhila inyuma ni ngona yaliyivuta kusubhila mumazi. Uko kuvutana kwaledeleyeje ukishikila ijosi ndyi mbuni ukwanza kureha. Kwi bahati yisole imbuni yalafanikiwa ukuvanamo umutwe wage mumunwa wi ngona. Mbuni yahweje nyiruka ugusubhira mwi poro ni josi dyage dyaweje lireha. Ubhugenzi bwage ni ngona bwafyiliye uwo musi na kuanzila ngaho imbuni yahweje ibhana ijosi lilishe mpaka ntya.
SHINGO YA MBUNI NA MAMBA
Fanani: hadithi!... Hadithi!.....
Hadhira : Hadithi njoo utamu kolea!.....
Hapo zamani za kale mbuni na mamba walikuwa marafiki wakubwa sana. Kila wakati mbuni alipokwenda mtoni alimsalimia mamba kwa mapenzi makubwa kabla ya kunywa maji. Mbuni alimthamini sana rafiki yake huyo. Ingawa mamba hula wanyama na ndege ila yeye hakuweza kumdhuru rafiki yake mbuni hata siku moja. Katika kipindi chicho mbuni alikuwa na shingo fupi tofauti na ilivyo sasa.
Kila siku mamba husubiri wanyama waje kunywa maji ili apate mlo wake kama kawaida yake. Hii ilikuwa ni kawaida yake kujificha majini na kuwasogelea wanyama hadi walipokuwa wanakunywa maji. Hapo alimrukia mnyama mmoja hadi walipokuwa wanakunywa maji. Hapo alimurukia mnyama mmoja na kumng’ata kwa meno yake na kumvuta majini kwenda kumlia huko. Baada ya shibe hutoka majini na kujilaza mcahngani kuota jua karibu na mto.
Basi, siku moja mamba alikuwa na njaa, siku hiyo alitegemea wanyama waje kama kawaida yake. Lakini kwa bahati mbaya hakuna mnyama hata mmoja aliyekuja kunywa maji. Njaa ya ajabu ilimshika mamba asijue cha kufanya. Alipokuwa katika hali hiyo alimuona rafiki yake mbuni akija. Sina njia nyingine isipokuwa kumshika mbuni na kumla ili kuzima njaa iliyonishika, mamba aliwaza. Mbuni alimsogelea rafiki yake na kumsalimia kama kawaida na kutambua kuwa mamba hakuwa na furaha yake ya kawaida. Mbuni nasema,
Mbuni : “Rafiki yangu mamba una nini?”
Mamba : kwa nini? (kwa sauti ya chini na unyonge)
Mbuni : Naona huna raha kabisa
Mamba : Jino linanisumbua sana
Mbuni : Jino?
Mamba : Ndiyo, nilikua nilikuwa nimekusubiri tu uniangalie na kuniambia hali ya jino
Mbuni, : oooh! Pole sana, basi fungua kinywa niangalie.
Mamba : ndiyo rafiki yangu jino la mwisho kabisa,
Mbuni alikiingiza kichwa chake ndani kuliangalia jino la rafiki yake mamba. Mara tu alipofanya hivyo, mamba alikifumba kinywa chake na kuanza kujivuta kurudi majini. Mbuni naye alijitahidi kufurukuta. Alijitahidi kwa nguvu zake zote kurudi nyuma.Kadri mbuni alivojivuta kuelekea nyuma ndivyo mamba alivyojivuta kuelekea majini kinyumenyume. Mvutano huu uliendelea mpaka shingo ya mbuni ikawa inarefuka. Kwa bahati mbuni alifanikiwa kufurukuta na kukitoa kichwa chake kwenye kinywa cha mamba. Mbuni alitimua mbio akirudi zake porini. Urafiki wake na mamba iliishia siku hiyu na tangua hapo mbuni akawa na shingo ndefu.


  1. Kisasili. Mfano wa kisasili katika lugha ya Kisukuma
SHANDYO SHA NYANZA YA NG’WANZA.
Nganji : Kalagu...
bhadegeleki :Kize!
Oliho ngikulu, olinang’witunja okwe na bhaniki bhabhili. Ungikulu ng’wenuyu ofugage ndilo mluzoga ulolwikalage guchumba lukundikijije. Indilo shinisho ojitumilage giti ikubhi ulushigu bhakumbulaga ndilo. Bhaadaye ung’witunja utola nkima, ungikulu ubhiza opandika ng’winga nanhwe aladamanile imijilo ya hakaya yiniyo, ubhiza ungikulu wandya guntongela imijilo ya henaho ili imane nanhwe ung’winga.
Lushigu lumo ungikulu na bhaniki bhakwe bhamla guja kujusena nhwi ng’wipolu ja guzugila, ungikulu ubhiza onagija ung’winga azuge shagulya sha limi. Ung’wila alazubhule indilo umluzoga ila asizibha ugulukundikija. Nhana ung’winga wandyaguhyagija gupyagula numba na goja shiseme sha kuzugila. Bhaada ya henaho uja gujuzubhula ndilo umluzoga, ahoomala guzubhula wibha ugukundikija ahaluzoga uja gujendeleya na milimo yakwe ya guzuga bhila gwizuka giki adalukundikijije uluzoga.
Ogimanila obhona minzi alokala umnumba andya gusambala pye ilibala lya heneho ahakaya. Yeeeeh! Wizuka giki adalukundikijije uluzoga lo ndilo. Wandya gutula ng’wano, pye abhanzengo bhandya gushangaa ugubhona minzi okalaga pye ilibala, bhamla bhuling’wene andye gwibhegeja gwikombola inholo yakwe ila nduhu uyo agafanikiwa.
Ungikulu na bhaniki bhakwe bhalinga ugunhwi bhushangaa ugubhona pye unzengo gobho gokala minzi na angi atali ongezeka kusambala. Uyomba ungikulu, “Hiiiiii!, ung’winga one wibhaga ugukundikija ahaluzoga lone, otumala gete”. Ahoomala kuyomba shinisho, ung’weyi na bhaniki bhakwe bhutibhila na gutibhila pye abhose. Lyubhiza lyokala minzi pye ilibala. Ishinisho hi shandyo sha Nyanza ya Ng’wanza.






ASILI YA ZIWA VIKTORIA
Fanani: Hadithi hadithi...
Hadhira :Hadithi njoo; tena njoo; na utamu kolea.!
Hapo zamani za kale palikuwepo na bibi mmoja ambaye alikuwa na mtoto mmoja wa kiume na wawili wa kike. Huyu bibi alikuwa akifuga samaki kwenye mtungi ambao ulikuwa umewekwa chumbani na haufunguliwi ovyoovyo. Samaki hao walitumika kama mboga siku bibi akijisikia. Baada ya mtoto wake wa kiume kuoa mke, bibi akawa amepata mwali ambaye hakufahamu sheria na taratibu za familia ile hivyo bibi huyu akawa na jukumu la kumwelekeza na kumfundisha taratibu za nyumbani pale.
Siku moja bibi pamoja na binti zake walipanga safari ya kwenda kutafuta kuni za kupikia, hivyo akamwachia mwali wake jukumu la kuandaa chakula cha mchana ambapo alimwagiza kuwa achukue samaki kutoka kwenye mtungi wake lakini asisahau kufunika. Mwali akaanza harakati za kufanya usafi wa nyumba pamoja na kuosha vyombo vya kupikia. Baadaye mwali akaenda kuchukua samaki kwenye mtungi na alipomaliza tu kuchukua wale samaki aliohitaji akasahau kuufunika ule mtungi wa samaki. Akaendelea na kazi zake za mapishi bila kukumbuka kama hajafunika mtungi.
Ghafla akaona maji yanajaa ndani ya nyumba na hatimaye yakazidi kusambaa eneo lote la pale nyumbani. Looo! Alikumbuka kuwa hakuufunika ule mtungi wa samaki. Akaanza kupiga kelele , watu wote pale kijijini wakashangaa kuona maji yanazidi kutanda kila sehemu jambo ambalo liliwafanya waanze kuhangaika kuzinusuru nafsi zao bila mafanikio yoyote.
Bibi na binti zake wakiwa wanatoka huko kuokota kuni walishangaa kuona eneo lote la kijiji chao limejaa maji na bado yanazidi kuongezeka. Yule bibi akasema, “ Oooooh! mwali wangu hakuufunika mtungi wangu, ametuteketeza”. Baada ya kusema hivyo, yeye na binti zake wakatitia wote na eneo lote likawa limejaa maji. Huo ndio mwanzo wa kutokea kwa Ziwa Viktoria.




  1. Maigizo. Mfano wa igizo la matambiko katika lugha ya Kisukuma
TAMBIKO LYA KUMALA MAKOYE
(Bhanazengo bhalibhonekana bhatebhayegu, bhuli ng’wene widimaga itama. Untemi alihang’wakwe atumanaga isho shilendelea).
Ng’wanazengo 1: Bhabehi nibholi amakoye gakwilile geke umzengo gwise? Mbula nduhu, mitugo jilegaiwa minze, shiliwa nduhu, nange hung’wisho go wolelo!
Bhanazengo bhose: (bhohaya) ilidakilwa tuntume njumbe ng’wa Ntemi akang’wele pye aya na tumane ung’wei aliganika ginehe.
Njumbe: (Wingila ng’wa Ntemi na kwandya mahoya). Nkulu Ntemi Mashimba, gite umo ulibhonela amakoye umzengo gwise gatushilaga, ki shandyo sha genaya pye?
Ntemi: Nunene natumanaga, kulwanguno haho obyalila unke wane mabhasa bhuyegu bhone bhushila.
Nshauri: Nkulu Mashimba, ilidakilwa tukamone Ntabiri atulokeje shandyo sha genaya pye, naki twite tulikane nago.
Ntemi: Iganiko lya wiza. Tumaga bhayanda bhakang’witane u Ntabiri (Lunduma).
Ntabiri: Niza nkulu Ntemi, nazunije ukukwambilija kulwanguno bhugota wa henaha bhudo no ila bhudakile bhuzunya wako.
Ntemi: Nazunije. Natuyegaga na makoye genaya umzengo gwane.
Ntabiri: Isho shilekoya habhana bhako mabhasa gite umo umanilile amasamva gise gatadakile mnho oseose umzengo gwise kubyala mabhasa. Ulu ulidaka gashile amakoye genaya Doi alidakilwa afunywe akaponywe mwiporu lya Giningi. Ugwenuyo gukubhi ng’wisho gwa makoye pye.
Ntemi: Nke wane mochage u Doi ung’wine Lunduma, ubhebhe ushoke mnumba abhise tuje nahwe ung’wiporu.
(Aho bhashika ukwiporu, Lunduma umocha u Doi na kuyomba mihayo ya kulomba kuzuniwa kafara yabho. Umocha na kunaja higolya ya liwe litale na kunsesebhela mininga ga mbuli yape. Aho wamala ubhahamilija pye abhanazengo kwinga bila kugaluka numa. Aho bhamala ukutambika pye makoye gushila hangi nubhuyegu bhushoka hange umzengo go Nyaluhande).




TAMBIKO LA KUONDOA MATATIZO
(Wanakijiji wanaonekana wakiwa hawana furaha, kila mmoja kashika shavu. Mtemi yupo kwake akiwa hajui nini kinaenedelea).
Mwanakijiji 1: Jamani mbona matatizo yamekithiri katika kijiji chetu? Mvua hainyeshi, mifugo inakosa maji na malisho, vyakula hakuna, au ndo mwisho wa dunia!
Wanakijiji wote: (wanadakia) inabidi tumtume mjumbe kwa Ntemi akamweleze haya yote na tujue yeye anafikiria nini.
Mjumbe: (akibisha hodi kwa Ntemi na kuanza mazungumzo). Mtukufu Mtemi Mashimba, kama unavyoona matatizo katika kijiji chetu hayaishi, nini chanzo cha haya yote?
Mtemi: Mimi mwenyewe sijui, maana tangu mke wangu ajifungue mapacha furaha yangu ilidumu kwa muda mfupi.
Mshauri: Mtukufu Mashimba, inabidi tukamuone mtabiri Lunduma atuonyeshe chanzo cha haya yote na nini tufanye ili kuepukana nayo.
Mtemi: Wazo zuri. Tuma vijana wakamuite Lunduma.
Lunduma: Ndio mtukufu, nimeitika wito wako na niko tayari kukusaidia kwani tatizo hili suluhisho lake ni dogo sana ila linahitaji utayari wako.
Mtemi: Niko tayari. Hata mimi sifurahishwi na matatizo katika kijiji changu.
Lunduma: Tatizo kubwa ni hawa watoto wako mapacha kwani kama ujuavyo mizimu ya mababu zetu haikubali mtu yeyote katika kijiji chetu kuwa na watoto mapacha. Hivyo inabidi Doto atolewe kafara kwa mizimu ya kijiji katika msitu wa Gingili na huo utakuwa mwisho wa haya yote.
Mtemi: Mke wangu mbebe Doto umkabidhi kwa Lunduma harafu wewe urudi ndani sisi twende naye msituni kwa ajili ya kukamilisha shughuli hii.
(Walipofika porini waliekea kwenye jiwe kubwa wakiwa wamechukua na mbuzi kwa ajili ya kupata damu itakayoandamana na kafara ya Yule mtoto. Mtabiri anambeba Doto na kunena maneno yanayoshiria kuomba kukubaliwa kwa kafara yao. Baadae anamnyanyua Doto na kumweka juu ya lile jiwe kubwa, kisha inaletwa damu ya Yule mbuzi na kunyinyiziwa Doto mwili wote akiwa am ekarishwa pale kwenye jiwe. Baada ya hapo mtabiri anawaamuru wanakijiji wote waliokuwepo pale waondoke lile eneo bila kugeuka nyuma kama ulivyo utaratibu wao kila wamalizapo tambiko. Baada ya kurejea nyumbani, hali ya hewa kijijini pale inabadilika na kuwa shwari kabisa, kwani wingu zito linatanda kuashiria uwepo wa mvua. Furaha inarejelea katika kijiji cha Nyaruhande).


4 comments:

  1. Maisha yangu Maajabu yanashangaza ushuhuda, Jinsi nimepata kisanduku chenye nguvu sana ambacho sasa ni pesa yangu mara mbili kutoka mia hadi elfu ya pesa ndani ya masaa 24, na pia jinsi nimerudisha mpenzi wangu wa zamani, sababu kuu niliwasiliana na Dk Lomi kwa msaada mimi kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, basi ananisaidia ni nguvu kubwa ya kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, na ananipenda na ananithamini sasa, basi mimi na Dr Lomi tukawa marafiki, baada ya mazungumzo kadhaa namuuliza ikiwa kuna njia anaweza kuniganga ili nipate pesa, hapo ndipo aliponiambia juu ya sanduku hili la uchawi, akaniambia kuna aina na saizi tofauti ya sanduku, aliniambia aina zote za sanduku, ningeweza kumudu ndogo tu ya sanduku, baada ya maombi muhimu anayofanya kwenye sanduku, ananipeleka kupitia huduma ya kujifungua, aliniambia niweke pesa ndani, niliweka ndani ya sanduku 100 euro baada ya masaa 24 nikagundua ilikuwa elfu 10 euro ndani, na nimekuwa nikitumia sanduku kwa miezi 7 sasa, mimi na mchumba wangu tunaishi maisha bora, ikiwa unahitaji b ack mpenzi wako au pesa spell wasiliana na Dr Lomi kwa barua pepe: lomiultimatetemple@gmail.com au WhatsApp namba +2349034287285 unaweza pia kumwandikia kupitia Jina la Mtumiaji la Snapchat: drlomi20 atakusaidia nje, asante kwa kusoma

    Kwaheri Gerd Ulrich

    ReplyDelete
  2. Sikuamini kuwa ningeweza kuungana tena na mpenzi wangu wa zamani, nilipatwa na kiwewe nikiwa nimesimama peke yangu bila mwili kusimama na mimi na kuwa nami, lakini nilipata bahati sana siku moja nilikutana na mchawi huyu wa hodari Dk. ASUBUHI, baada ya kumueleza hali yangu alifanya kila liwezekanalo kumuona mpenzi wangu anarudi kwangu, kweli baada ya kunifanyia uchawi mpenzi wangu wa zamani alirudi kwangu chini ya masaa 48, mpenzi wangu wa zamani alirudi akiniomba kuwa hatawahi. niache tena, miezi 3 baadaye tulioana na kuoana, ikiwa pia una hali sawa. Ana nguvu nyingi katika mambo yake;
    *penda uchawi
    * kama unataka ex wako nyuma
    * Acha talaka
    *kuvunja mawazo
    * huponya viharusi na magonjwa yote
    * uchawi wa ulinzi
    *Ugumba na matatizo ya ujauzito
    Wasiliana na Dk DAWN kwa barua pepe yake: dawnacuna314@gmail.com
    Whatsapp: +2349046229159

    ReplyDelete
  3. Mume wangu amerudi!!! Baada ya miaka 1 ya ndoa iliyovunjika, mume wangu aliniacha na watoto wawili na maisha yangu yalivunjika. Nilitaka kuyamaliza, nusura nijiue maana alituacha bila chochote. Nimekuwa nimevunjika kihisia wakati huu wote na maisha yanaonekana kutokuwa na maana. Siku moja mwaminifu, nilipokuwa nikivinjari mtandao, nilikutana na baadhi ya shuhuda kuhusu Dk DAWN. Baadhi ya watu walishuhudia kwamba alimrudisha mpenzi wao wa zamani, wengine walishuhudia kwamba anarejesha tumbo na kuponya magonjwa kwa mimea. Nilipendezwa zaidi na upatanisho na mume wangu, ambao Dk. DAWN aliwezesha kumrudisha mume wangu ndani ya siku 3. Sasa mume wangu amerudi na tumekuwa tukiishi kwa furaha tangu wakati huo. Shukrani zote kwa Dk DAWN. Hapa, ninaacha mawasiliano yake kwa kila mtu. Maana kuna changamoto za aina yoyote,
    Barua pepe ( dawnacuna314@gmail.com )
    Whatsapp: +2349046229159

    ReplyDelete
  4. Kwa zaidi ya miaka 13 ya ndoa sikuweza kuzaa, naendelea kuharibika hata nikipata mimba, madaktari wote hawakuweza kunisaidia, hadi dada yangu akanielekeza kwa Dr DAWN, ambaye alinisaidia nikapata ujauzito na sasa hivi kuwa na mtoto mzuri wa kike,
    Anasaidia pia marafiki zangu wengi niliowaelekeza, Dr DAWN ni baraka kwa kila mtu anayewasiliana naye,
    *Kama unataka kupata mimba.
    *Ukitaka kuacha kuharibika kwa mimba.
    *Ukitaka kumrudisha mpenzi wako.
    *Kama unataka mume/mkeo arudishwe.
    *Kama unataka kurejesha mali yako iliyoibiwa au Pesa.
    *Ukitaka kutibu aina yoyote ya ugonjwa,
    Wasiliana naye kwa WhatsApp: +2349046229159

    ReplyDelete

hakiki na tuma maoni au mapendekezo kuhusu makala hii ya andiko langu la uchunguandiko langu

ANDIKO LA UCHUNGU (Kwa shemeji zangu na wanangu)           NYAMBUYA OGUCHU,                            S.L.P 777666,       ...